KARIBUNI KWENYE BLOG YANGU ILI USIPITWE NA HABARI KEMKEM,KWA HABARI MOTOMOTO NDANI NA NJE YA NCHI MICHEZO NA BURUDANI NA ZINGINEZO NYINGI UNGANA NAMI NICK 4REAL

Saturday, October 12, 2013

FUNGUA HAPA UONE SHULE INAYOONGOZA KWA WANAFUNZI KUPATA MIMBA MKOANI MBEYA

Mkuu  wa  mkoa wa Mbeya Bw  Abas Kandoro
 SHULE ya Sekondari, Stephen Kibona iliyopo wilayani Ileje mkoani Mbeya, imetajwa kuwa ni moja ya shule vinara kwa wanafunzi wa kike kupata mimba.
Baadhi ya walimu wanaofundisha na waliowahi kufundisha katika shule hiyo, wameyasema hayo wakati wamepiga simu kuomba waandishi wa habari kufuatilia zaidi mimba za utotoni kwa wanafunzi baada ya kusoma makala isemayo mimba za utotoni tatizo Mbeya, Pwani na Mara
Walimu nhao wamesema kuwa, kwa mwaka mmoja katika shule hiyo si chini ya wanaunzi 10, wanaoacha masomo huku wazazi wa wanafunzi hao wa kike na kiume wanaowapachika mimba wakishirikiana kuzima dhambi hiyo.
Hivi karibuni, Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, aliwahi kusema kuwa wazazi watakaoshirikiana kuhusika kuwatorosha wanaowapa mimba wanafunzi wangeweza kuchukuliwa hatua.
CHANZO;HABARI MPASUKO

No comments :

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...